Informações:
Sinopse
Makala ya Wimbi la Siasa inakupa fursa ya kufahamu masuala ya kisiasa yanayoendelea ndani na nje ya Bara la Afrika. Kwenye Makala haya utapata habari ambazo zinakugusa moja kwa moja wewe msikilizaji. Kila wakati usikose kusikiliza Makala ya Wimbi la Siasa
Episódios
-
Mazungumzo mapya kati ya waasi wa M23/AFC na serikali ya DRC nchini Uswizi
15/04/2026 Duração: 10minAwamu ya tisa ya mazungumzo ya amani kati ya waasi wa M23/AFC na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, yalianza siku ya Jumatatu Aprili 13 nchini Uswizi. Ujumbe wa Qatar ambao ni wasuluhishi, akiwemo mjumbe wa Marekani kuhusu masuala ya Afrika Massad Boulos, wanashiriki. Nini Ajenda ya mazungumzo haya ? Raia wa DRC wategeme nini ? Tunachambua.
-
Harakati za watetezi wa haki za binadamu Mashariki mwa DRC
08/04/2026 Duração: 09minMashirika ya kutetea haki za binadamu yakiongozwa na Amnesty International, katika ripoti zao, yamekuwa yakionya kuwa maisha ya wanaharakati wa haki za binadamu, wana habari na viongozi wa mashirika ya kiraia yapo hatarini katika maeneo yanayodhibitiwa na waasi wa M23, Mashariki mwa DRC. Wiki hii Ruben Lukumbuka, anazungumza na Jack Sinzaera, mwanaharakati maarufu kutoka Kivu Kaskazini.
-
Viongozi wa ODM wanaweza kuungana tena baada ya mpasuko wa chama ?
01/04/2026 Duração: 10minChama siasa cha Orange Democratic Movement-ODM kinaendelea kugawanyika, kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2027 nchini Kenya. Tangu kufariki dunia kwa Raila Odinga, mwasisi wa chama hicho kikubwa cha upinzani, viongozi waandamizi wa ODM wameshindwa kuelewana kuhusu kuendelea kumuunga mkono rais William Ruto, anayetarajiwa kuwania tena urais kwa muhula wa pili. Nini hatima ya chama hiki ?
-
DR Congo: Ni wakati mwafaka wa kuibadilisha katiba ya DRC ?
25/03/2026 Duração: 10minMjadala wa kuibadilisha katiba nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, umepamba moto. Wanasiasa wanaoegemea upande wa rais Felix Tshisekedi na chama chake cha UDPS wanaunga mkono mchakato wa katiba kubadilishwa. Upinzani wakiongozwa na naibu Spika wa Bunge la Seneti aliyejiuzulu Modeste Bahati Lukwebo, unapinga. Ni wakati mwafaka wa kuibadilisha katiba ya DRC ?
-
Nini hatima ya vita vya Marekani na Israeli nchini Iran ?
18/03/2026 Duração: 10minNi wiki ya tatu sasa, baada ya Marekani na Israeli zilipoanza kutekeleza mashambulizi ya kijeshi nchini Iran. Mataifa hayo mawili yanasema lengo la mashambulizi hayo ni kuhakikisha kuwa inaharibu kabisa miundo mbinu ya Iran kutengeneza silaha za nyuklia. Rais wa Marekani Donald Trump, anasema vita hivi vitamalizika hivi karibuni, lakini haifahamiki ni lini. Tunachambua.
-
Kenya: Je, ushirikiano wa serikali kati ya vyama vya ODM na UDA unafanikiwa ?
11/03/2026 Duração: 10minUmepita mwaka mmoja tangu chama tawala nchini Kenya UDA na kile cha upinzani ODM, vilipoingia kwenye makubaliano ya kisiasa na kutaja mambo 10 kama vita dhidi ya ufisadi, kupunguza deni la taifa, ujumuishwaji ulio sawa serikalini kama baadhi ya mambo ya kushughulikia baada ya maandamano ya vijana ya mwaka 2024. Je, mwaka mmoja baadaye mambo hayo yametekelezwa kwa kiasi gani ? Tunachambua.
-
Nini hatima ya vita vya Israel na Marekani nchini Iran ?
04/03/2026 Duração: 10minDunia inashuhudia vita katika ukanda wa Mashariki ya Kati, baada ya Marekani na Israeli kuishambulia Iran, tangu Februari 28. Rais wa Marekani Donald Trump na Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu wanataka Iran iache kutengeneza silaha za maangamizi, kuyaunga mkono makundi yenye silaha nje ya Iran na kubadilisha utawala. Kongozi wa kiroho Ayatolla Ali Khamenei, ameuawa katika vita hivyo. Nini hatima ya vita hivi ? Tunachambua.
-
Vita vya miaka minne nchini Ukraine, nini suluhu ?
25/02/2026 Duração: 09minImetia miaka minne, tangu Urusi ilipoivamia Ukraine, katika vita vikubwa tangu vile vya pili vya dunia barani Ulaya. Maelfu ya watu wameuawa, miji na miundo mbinu muhimu imeharibiwa nchini Ukraine. Rais Volodymyr Zelenskyy anasema mwenzake wa Urusi hajatimiza malengo yake ya vita. Kwanini suluhu haijapatikana miaka minne baadaye ?
-
Kenya: Kwanini chama cha ODM kimegawanyika kuelekea uchaguzi mkuu 2027 ?
18/02/2026 Duração: 10minJoto la kisiasa limeendelea kupanda kwenye chama cha siasa cha ODM nchini Kenya kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2027. Chama hicho kilichoanzishwa zaidi ya miaka 20 iliyopita na aliyekuwa Waziri Mkuu Marehemu Raila Odinga, kimegawanyika kwa makundi mawili. Kundi moja linaongozwa na Oburu Oginga, kaka yake Raila, linamuunga mkono rais William Ruto. Kundi lingine, linangozwa na Edwin Sifuna, Katibu Mkuu anayempinga Ruto. Nini hatima ya chama hiki ?
-
Nini kikwazo cha utekelezwaji wa mkataba wa kusitisha vita nchini DRC ?
11/02/2026 Duração: 10minWawezeshaji na wasuluhishi wa mzozo wa Mashariki mwa DRC kutoka Umoja wa Afrika, wanataka usitishwaji wa vita na utekelezwaji wa mkataba wa amani wa Washington na kuheshimu mchakato wa Doha. Ni kwanini inakuwa vigumu kutekeleza mkataba huo kuheshimu maelewano ya Doha ? Tunachambua.
-
Mazungumzo ndio suluhu ya changamoto zinazoikabili DRC ?
04/02/2026 Duração: 10minRais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Felix Tshisekedi amesema serikali yake ipo tayari kuongoza mazungumzo kati ya Wakongomani, ili kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili nchi hiyo, hasa utovu wa usalama, mashariki mwa nchi hiyo. Hata hivyo, Chama cha "Ensemble pour la République, kinachoongozwa na mwanasiasa mashuhuri wa upinzani Moise Katumbi, kinasema mazungumzo hayo yanaweza kufanyika tu iwapo yatawashirikisha wadau wote. Rais Tshisekedi, wanaotekeleza mauaji ya raia, hawapaswi kushirikishwa kwenye mazungumzo hayo. Tunachambua.
-
Kenya: Nini suluhu ya mzozo wa chama cha ODM ?
28/01/2026 Duração: 10minChama cha ODM kilichoanzishwa na aliyekuwa Waziri Mkuu nchini Kenya Hayati Raila Odinga, kinapitia mgawanyiko wa kisiasa kuhusu kumuunga mkono rais William Ruto kuwania urais kwa muhula wa pili. Viongozi wa chama hicho wamegawanyika kuhusu mpango huo kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2027. Mvutano huu unamaanisha nini ?
-
Uganda: Museveni achaguliwa tena baada ya miaka 40 madarakani
21/01/2026 Duração: 10minRais Yoweri Museveni, mwenye umri wa miaka 81, na ambaye amekuwa madarakani kwa miaka 40, alitangazwa mshindi wa uchaguzi mkuu wa Januari 15 baada ya kupata asilimia 71.65 ya kura. Mpinzani wake wa karibu Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine mwenye umri wa miaka 43, alimaliza wa pili kwa kupata asilimia 24.72 ya kura. Bobi Wine amedai kuibiwa kura. Ushindi wa rais Museveni unamaanisha nini ?
-
Uganda: Je, uchaguzi mkuu utakuwa huru na haki ?
14/01/2026 Duração: 09minUchaguzi wa wabunge na urais nchini Uganda unafanyika Januari 15, 2026. Rais wa muda mrefu Yoweri Museveni ambaye ameongoza kwa miaka 40, anapambana tena na mpinzani wake mkuu Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine. Upinzani umelalamikia kunyanyaswa, wakati huu mtandao wa Interneti ukizimwa. Je, uchaguzi huu utakuwa huru na haki ? Tunachambua kutoka Kampala.
-
Kutekwa na kufunguliwa mashtaka kwa Maduro nchini Marekani kunamaanisha nini ?
07/01/2026 Duração: 10minRais Donald Trump, Januari 3, 2026, aliagiza operesheni maalum ya wanajeshi wa Marekani nchini Venezuela, kumteka kiongozi wa nchi hiyo Nicolas Maduro. Baada ya kitendo hicho ambacho kimelaaniwa duniani, Maduro alisafirishwa jijini New York na kufunguliwa mashtaka ya kuongoza biashara haramu ya dawa za kulevya nchini Marekani. Tunachambua hatua hii ya rais Trump, inamaanisha nini ?
-
Matukio makubwa ya kisiasa yaliyotikisa Afrika Mashariki na Kati mwaka 2025
31/12/2025 Duração: 10minMatukio makubwa ya kisiasa tuliyochambua mwaka 2025 ni pamoja na kifo cha aliyekuwa mwanasiasa mashuhuri nchini Kenya Raila Odinga, uchaguzi wenye vurugu uliofanyika nchini Tanzania Oktoba 29 na kutiwa saini kwa mkataba wa kumaliza vita Mashariki mwa DRC, Desemba 04, jijini Washington DC nchini Marekani.
-
DRC: Kuondoka kwa waasi wa M23/AFC mjini Uvira kunamaanisha nini ?
24/12/2025 Duração: 09minBaada ya shinikizo kutoka kwa Marekani, waasi wa M23/AFC waliondoka kwenye mji wa Uvira, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Hata hivyo, rais Felix Tshisekedi ameelezea kitendo hicho kama kiini macho kwa jumuiya ya Kimataifa, kauli ambayo imeungwa na mkono na jeshi la FARDC wanaosema, waasi hao wamejificha katika milima inayopatikana na mji huo. Kuchambua kinachoendelea, tunaungana Mali Ali akiwa jijini Paris na François Alwende akiwa jijini Nairobi.
-
DRC: Nini hatima ya Uvira baada ya M23/AFC kuuteka mji huo ?
17/12/2025 Duração: 10minHali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, si shwari licha ya kutiwa saini kwa mkataba unaolenga kusitisha vita ambavyo vimekuwa vikiendelea kwa muda wa miaka 30. Waasi wa M23/AFC wameudhibiti mji wa Uvira. Marekani inaonya kuichukulia hatua Rwanda kwa kuwaunga mkono waasi hao ambao sasa wameahidi kuondoa vikosi vyake katika mji huo, lakini kwa masharti. Tunachambua kwa kina.
-
Wanasiasa wa upinzani kukabiliwa na vurugu, Uganda
10/12/2025 Duração: 10minKampeni za uchaguzi nchini Uganda zimezidi kupamba moto kuelekea uchaguzi mkuu January 15 2025 ambapo Rais Yoweri Museveni aliyeingia madarakani mwaka wa 1986, anagombea tena muhula wa saba huku akishindana na wagombea wengine miongoni mwao mwanasiasa wa upinzani Robert Kyagulanyi Ssentamu almaarufu Bobi Wine. Kampeni za mwaka huu zinafanyika huku mgombea wa Upinzani Bobi wine akilalamika kushambuliwa na maafisa wa usalama. Kupata mengi zaidi ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka
-
Viongozi wa DRC na Rwanda kutia saini makubaliano ya amani, huko Washington DC
03/12/2025 Duração: 10minMakala ya wimbi la siasa, imeangazia hatua ya viongozi wa Rwanda na DRC ambao siku ya alhamisi desemba 04 watatia saini makubaliano ya amani, mbele ya rais wa Marekani Donald Trump hii ikiwa ni mwendelezo wa mapatano ya amani mashariki mwa DRC yaliyosimamiwa na Marekani yaliyotiwa saini na mawaziri wa mambo ya nje wa nchi hizo mbili juni 27. Profesa Pacifique Malonga ni mchambuzi wa siasa akiwa Kigali Rwanda, pia Francois Alwende ni mtaalamu wa siasa za maziwa makuu akiwa Nairobi Kenya.