Wimbi La Siasa

Harakati za watetezi wa haki za binadamu Mashariki mwa DRC

Informações:

Sinopse

Mashirika ya kutetea haki za binadamu yakiongozwa na Amnesty International, katika ripoti zao, yamekuwa yakionya kuwa maisha ya wanaharakati wa haki za binadamu, wana habari na viongozi wa mashirika ya kiraia yapo hatarini katika maeneo yanayodhibitiwa na waasi wa M23, Mashariki mwa DRC. Wiki hii Ruben Lukumbuka, anazungumza na Jack Sinzaera, mwanaharakati maarufu kutoka Kivu Kaskazini.